Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2022

VIJANA

  NINI MATARAJIO YA MUNGU KWA VIJANA  1yohana 2:14 “…. Nimewaandikia ninyi,vijana kwa sababu mna nguvu,na neno la Mungu linakaa ndani yenu ,nanyi mmeshinda yule mwovu.”Mungu anao mtazamo wake binafsi juu ya kila kundi la watu chini ya jua,.Na kila kundi mfano wa wamama,wajane,watoto,vijana kuna mambo fulani ambayo Mungu anatarajia kila kundi litatekekleza. Mungu anazungumza na vijana na kusema nimewaandikia ninyi vijana kwa sababu moja mna nguvu,mbili neno la Mungu linakaa ndani yenu, na tatu mmemshinda yule mwovu. Nguvu zinazozungumziwa hapa ni nguvu,uweza wa Mungu wa kukusaidia kutekeleza maagizo yake. Na kwa sababu hiyo basi kuna matarajio ya Mungu kwa hao vijana. Sasa lengo la ujumbe huu mfupi ni kukueleza nini Mungu anatarajia/anategemea kwamba utafanya sawasawa na nafasi aliyokupa mbele zake na uwezo aliokupa. Matarajio ya Mungu kwa vijana ni kama ifuatavyo: *Moja, Vijana wauteke ufalme wake. Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupa...

IMANI NA MAOMBI

  UHUSIANAO WA IMANI NA MAOMBI. UTANGULIZI: IMANI NINI? Imeandikwa  WAEBRANIA 11:1 "Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo ni bana ya mambo yasiyoonekana." Yesu ndiye mwanzo wa imani imeandikwa LUKA 17:5 "Mitume wakamwambia Bwana tuongezee imani." WARUMI 10:17 yasema "Basi imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la kristo." Imani ya haki ni kuamini yote ambayo Yesu ametutendea. imeandikwa WARUMI 5:1 "Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na imani kwa Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu kristo." Imani ni kuwa na imani kwa Mungu katika mambo yote. imeandikwa WAEBRANIA 10:38 "Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani naye akisita-sita Roho yangu haina furaha naye." Imani dhaifu yaweza kuwa yenye nguvu Mungu akimsaidia imeandikwa MARKO 9:24 "Mara babaye yule kijana akapaza sauti akasema Naamini nisaidie kutokuamini kwangu." Mwombaji yeyeote ili awe na nidhamu katika Maombi ni lazima a...